16th April, 2019
Mkufunzi wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba Paul Murunga amesema kwamba licha ya kutofikia malengo yake ya kutinga robo fainali ya kombe kuu kwenye mashindano ya msururu wa raga duniani mkondo wa singapore, ameridhishwa na matokeo ya timu hiyo kwani alifanya vyema singapore zaidi ya mkondo wa Hong Kong.