.
16th March, 2019
Baadhi ya viongozi kutoka katika Kaunti ya Wajir wamekashifu kuhamishwa kwa Waziri Amina Mohamed kama waziri wa elimu na wadhifa wake kukabidhiwa profesa george magoha.wakiongozwa na mbunge wa wajir east rashid kassim, viongozi hao wametaja mabadiliko ya hivi juzi yaliofanywa na rais uhuru kenyatta katika baraza la mawaziri kama hujuma kwa jamii ya kuhama hama na wametishia kuwashinikiza wabunge wenzao kutoidhinisha uteuzi wa magoha. Wanadai magoha hakuwajibika alipokuwa mwenyekiti wa baraza la kitaifa la mitihani nchini.