16th March, 2019
Wakenya Simon Ngige na Justus Madoya walifuzu kwenye raundi ya tatu na ya mwisho ya mashindano ya gofu ya Kenya Open yanaoyoendelea uwanjani karen country club jijini Nairobi. Adri Arnau na gudo miliotsi walichukua usukani wakielekea kwenye raundi ya mwisho baada ya kumpiku Louis de Yager ambaye amekuwa akiongoza kutoka mashindano hayo yang'oe nanga siku ya Alhamisi. Arnau na Miliotsii kwa sasa wanashikilia nafasi ya kwanza kwenye jedwali la mashindano hayo wakiwa na alama 14.