12th March, 2019
Timu ya taifa ya soka Harambee stars imenufaika pakubwa baada ya kupata ufadhili wa shilingi milioni 20 kutoka kwa kampuni ya mchezo wa bahati nasibu ya Betin. Rais wa shirikisho la soka nchini Nick Mwendwa amesema kwamba pesa hizo zitatumika katika maandalizi ya timu hiyo kwenye dimba la soka barani Afrika.