15th February, 2019
Mgomo wa wauguzi waingia siku ya 12, huku wakikaidi amri ya Rais Uhuru
Awamu ya hivi punde zaidi ya mgomo wa wauguzi imeingia siku ya kumi na mbili, wahudumu hao wa afya wakionekana kukaidi tisho la rais Uhuru Kenyatta la kuwatimua kazini. Mgomo huo umeathiri angalau kaunti 11, wauguzi wakidai marupurupu kwa mujibu wa mkataba wa maelewano na serikali wa mwaka 2017.