15th February, 2019
Gavana wa Wajir awasihi wapinzani kuungana naye kufanya maendeleo
Mahakama ya juu zaidi imebatilisha uamuzi wa mahakama ya rufaa iliyoharamisha ushindi wa gavana Mohamed Abdi katika uchaguzi wa Agosti 8 mwaka 2017. Mpinzani wake Ahmed Abdullahi alielekea mahakamani kupinga ushindi huo kwa madai kuwa stakabadhi zake gavana Abdi hazikuwa halali, aidha baada ya tangazo la leo gavana Abdi aliwarai wapinzani wake kushirikiana naye katika uongozi wa kaunti ya wajir ili kuhakikisha maendeleo yanazingatiwa.