11th February, 2019
Rais wa shirikisho la soka nchini Nick Mwendwa amethibitisha kwamba Mkufunzi wa timu ya taifa ya soka Harambee Stars Sebastian Migne , bado hajapokea mshahara wa miezi mitatu,ila ameahidi kwamba kocha huyo atapata mshahara wake shirikisho likipokea hela kutoka katika hazina ya michezo inatarajiwa kuanza mikakati ya kuachilia fedha hizo siku ya jumanne. Nick aliyazungumzia hayo na mengine mengi katika mahojiano na mwanahabari wetu robinson okenye, katika kipindi chetu cha michezo cha ktn scoreline siku ya jumapili.