.
5th February, 2019
Waziri wa Usalama wa ndani Dr. Fred Matiangi leo ameongoza mkutano wa mawaziri wote serikalini katika kile kinachozingatiwa kuwa ni utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya serikali. Lakini wachambuzi wanasema kuwa majukumu anayotekeleza kwa sasa waziri matiang'i ni yale ya waziri mkuu cheo ambacho hata hivyo hakitambuliwi na katiba. Hii ni baada ya uteuzi wake uliofanywa kupitia amri ya kisheria na rais uhuru kenyatta, ziporah syokau na taarifa zaidi.