5th February, 2019
Mkufunzi wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji 7 kila upande Paul Murunga amelaumu ukosefu wa wachezaji wazoefu kwenye kikosi kuwa chanzo cha matokeo duni kwenye michuano ya msururu wa raga wa Sydney. Kenya ilifungwa mechi zake zote tatu katika michuano hiyo.