30th January, 2019
Wakazi wa Kaunti ya Uasin Gishu watapata maji zaidi kwa lita milioni 20 baada ya kuanzishwa kwa mpango wa kutibu maji na serikali ya kaunti.
Jackson Mandago, gavana wa kaunti, hiyo amesema mradi huo wa kipkaren utasambaza maji maeneo ya Kapseret, Langas na Kipkenyo pamoja na maeneo yaliyo karibu na wadi hizo.
Mpango huo wa maji utahakikisha kuwa asilimia 85 ya maboma katika kaunti hiyo yana maji safi.