24th January, 2019
Kundi moja la wanaharakati sasa linamtaka mkurugenzi wa upelelezi nchini, DCI, George Kinoti, kuanzisha uchunguzi kwa kusudi la kumchukulia hatua ocs wa kituo cha polisi cha
Capitol Hill, kwa madai ya kufanya kazi kwa mapendeleo. Aidha kundi hilo kwa jina, concerned citizens alliance, linashinikiza kukamatwa kwa mwekezaji mmoja wa binafsi
Anayedaiwa kupanga njama ya kuvamia na kuharibu mali ya jirani yake kwa lengo la kunyakuwa ardhi yake. Ila hata baada ya ripoti kupigwa na wahusika kutambuliwa hapana
Mshukiwa yeyote aliyekamatwa na kushtakiwa