24th January, 2019
Mzozo wa uongozi umezuka katika muungano wa Waislamu jijini kisumu ambapo makundi mawili yametofautiana kuhusu mipango ya kufanya uchaguzi wa kuwaleta viongozi wapya ofisni. Mwenyekiti aliyepo kwa sasa sheikh musa alphan ameapa kutoruhusu uchaguzi wowote kufanywa licha ya amri ya mahakama kuamuru shughuli hiyo kufanywa. Wakati huohuo baraza la wasilamu nchini, supkem limeelezea kusikitishwa kwake na kukosekana kwa sajili ya wanachama wa muungano huo. Yusuf Ndicho, mmoja wa viongozi kwenye muungano huo aliwaambia wanahabari jana mjini kisumu kwamba ipo miskiti inayowasajili wanachama kinyume cha sheria kwa madhumuni ya kushiriki kwenye uchaguzi huo