24th January, 2019
Rais mpya wa jamhuri ya Demokrasia ya Congo Felix Tshisekedi anaapishwa rasmi alasiri hii katika jiji la Kinshasa. Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria utawazo huo akiandamana na kiongozi wa chama chaODM Raila Odinga na Kalonzo Musyoka wa wiper. Uapisho huo unakuja baada ya mahakama ya kikatiba nchini humo kukubaliana na ushindi wa Tshisekedi licha ya Martin Fayulu kupinga ushindi wake mahakamani. Rais tshisekedi mwenye umri wa miaka hamsini na mitano ni mwanaye aliyekuwa kiongozi mahiri wa upinzani nchini humo, marehemu etienne tshisekedi aliyefariki mwezi wa Februari mwaka wa 2017 akiwa na umri wa miaka themanini na minne