18th January, 2019
Kundi moja la wakulima huko Naivasha limetoa notisi ya siku kumi na nne kwa shirika la huduma za wanyama pori, KWS kushughulikia mgogoro kati yao na wanyama pori eneo hilo, la sivyo wachukue hatua mikononi. Wakulima hao katika kijiji cha mirera wanalalamikia wanyama pori wanaovamia mashamba yao na kuharibu mazao