18th January, 2019
Aliyekuwa afisa wa kitengo cha uagizaji katika huduma za vijana kwa taifa, NYS Selesio Karanja, amehukumiwa kifungo cha miaka minne gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika kwenye ulaghai katika sakata ya NYS. Hakimu lawrence mugambi alisema kwamba mshtakiwa karanja, atahitajika kulipa faini ya shilingi milioni 5 pia, baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha kesi dhidi yake bila shauku yoyote. Hakimu mugambi pia alisema kwamba baada ya mshtakiwa kukamilisha adhabu ya kifungo, hatoruhusiwa kuhudumu katika nafasi yoyote ya umma serikalini. Selesio karanja amekuwa mtuhumiwa wa kwanza katika sakata ya NYS