14th January, 2019
Mkuu wa polisi Joseph Boinett ametoa onyo kwa Maafisa wa akiba ?NPR wanaozembea kazini kwamba chuma chao ki motoni. Boinet amesema serikali imeweka mikakati kabambe ya kukabiliana na maafisa wanaodumaza huduma ya usalama aidha boinett alidokeza kuwa ipo haja ya kutafuta suluhu la kudumu kwenye mizozo baina ya jamii Zinazohasimiana kwa kutumia maendeleo kama kigezo muhimu cha kubadili mustakabali wa jamii zinazoishi kwenye maeneo Kame. Hata hivyo Boineet aliwataka wakaazi kushirikiana na polisi katika kuimaraisha usalama unaoshuhudiwa miongoni mwao. Boinet aliyasema haya huko bonde la Kerio.