14th January, 2019
Kiongozi wa chama cha Ford Kenya Moses Wetangula amesisitiza kuwa atakuwa debeni katika kinyangányiro cha urais wa 2022. Akizungumza akiwa Magharibi mwa Kenya amesema kwamba wakati huu ni wake wala hayuko radhi kumwachia yeyote nafasi hiyo pindi wakati huo utakapofika. Wetangula alikuwa mmoja wa viongozi wa muungano wa upinzani nchi NASA katika uchaguzi mkuu uliopita lakini akajitenga na kundi hilo baada ya kutofautina na aliyekuwa kinara wa kundi lao Raila Odinga