24th December, 2018
Bondia chipukizi kutoka kenya david kamala amejiunga na masumbwi ya kulipwa baada ya kushiriki katika ndondi za kujifunza. Kamala anatarajia kuimarika na kupata matokeo mazuri. Na ijapokuwa ameipata nafasi hii, bondia huyo anafahamu fika changamoto zinazomsubiri na yupo tayari kupambana nazo ima fa ima ili kupata mataji anayoyakamia.