17th December, 2018
Rais wa kizazi cha kesho maarufu future generation Jadiel Maina amemtaka rais Uhuru Kenyatta kutangaza saratani kama janga la kitaifa. Maina aliyasema hayo alipokuwa akizindua mpango wa kizazi salama na saratani au cancer free generation, kampeni inayopaniwa kuwapa matumaini watu wanaoishi na ugonjwa wa saratani sawa na kuweka mipango ya kudhibiti ugonjwa huo.