17th December, 2018
Kisa cha hapo jana ambapo afisa mmoja wa polisi huko Kolongolo kaunti ya Trans Nzoia anadaiwa aliwamiminia risasi na kuwaua watu watano, kimeshtumiwa na uongozi wa kaunti hiyo. Gavana Patrick Khaemba amekemea kisa hicho kilichowaacha watu wengine na majeraha, pale ambapo makabiliano yalizuka kati ya raia na maafisa wa polisi. Wito umetolewa wa hatua kuchukuliwa dhidi ya mhusika wahusika. Makabiliano hayo yalitokana na mzozo katika familia moja, ambapo polisi walipojaribu kuingilia kati, ndipo raia wakaanza kuwakaripia maafisa hao. Watu wawili walikufa papo hapo huku wengine watatu wakifariki walipokuwa wakipokea matibabu hospitalini.