15th December, 2018
Katibu wa Muungano wa Wafanyikazi COTU Francis Atwoli amesisitiza lazima kutakuwepo na mabadiliko ya kikatiba kabla ya uchaguzi wa mwaka 2022. Mabadiliko hayo yataleta usawa wa kiuongozi na kusuluhisha changamoto na mizozo ya kisiasa ambayo imekuwa ikishuhudiwa. Aliyasema hayo katika hafla ya mahafala ya chuo cha masinde muliro alipotuzwa na shahada kutokana na juhudi zake za kuleta hamasa kuhusu harakati za wafanyikazi nchini.