10th December, 2018
Watu watano wamefariki dunia papo hapo huku tisa wakipata majeraha mabaya katika ajali ambayo imefanyika katika eneo la malili kwenye barabara kuu ya Mombasa?Nairobi leo asubuhi. Kulingana na walioshuhudia ajali hiyo,ni gari binafsi la watu kumi na wanne lililokuwa limebeba watu wa kanisa moja lilikuwa likitoka upande wa Nairobi na lilogongana ana kwa ana na lori lililokuwa likitoka upande wa Mombasa na kusababisha vifo vya watu hao. Waliojeruhiwa wamepelekwa katika Hospitali ya Machakos level 5 kupata matibabu ya dharura nao maafisa wa trafiki wakiendelea kudhibiti hali ya usafiri kuhakikisha kwamba hakujashuhudiwa msongamano wa magari.