6th December, 2018
Kesi ya ufisadi kuhusu NaibuJjaji Mkuu Philomena Mwilu inasikizwa na majaji watano katika mahakama kuu. Majaji Hellen Omondi, Mumbi Ngugi, William Musyoka, Francis Tuiyot na Chacha Mwita walianza kusikiza kesi hiyo ambapo kiongozi wa Mshtaka ya Umma Noordin Hajji amemteua wakili wa malikia wa Uingereza khawar qureshi kuongoza kesi hiyo. Hajji aliiambia kamati ya seneti kuhusu sheria kwamba alichukua uamuzi huo baada ya mawakili wa humu nchini kuonekana kuogopa kushughulikia kesi hiyo. Wakili James Orengo anamwakilisha jaji Mwilu.