29th November, 2018
Aliyekuwa afisa mkuu mtendaji wa Tume ya Uchaguzi na Mipaka IEBC, Ezra Chiloba hivi leo amehojiwa kwa undani na Kamati ya Bunge, ya Kuchunguza Matumizi ya Fedha za Umma kuhusu jinsi zabuni ilitolewa ya kununua vifaa vya elektroniki kutoka kampuni ya Safran Morpho, kwa matumizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017. Chiloba ameiambia kamati hiyo kwamba mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati alisema uongo alipoiambia kamati hiyo kwamba uamuzi wa kununua vifaa hivyo ulifanywa na Chiloba pekee yake bila kuwahusisha makamishina.