29th November, 2018
Mwanamme mmoja mwenye umri wa miaka 24 ameuawawa kwa kupigwa kwa madai kuwa aliiba kuku wa jirani katika kijiji cha Lukhome eneo bunge la Kiminini kaunti ya Trans Nzoia. Taarifa zinasema kuwa kundi la vijana katika kijiji hicho walimpiga mwanamme huyo aliyetambuliwa kwa jina la Sammy Wabulakha wakimshurutisha asalimishe kuku waliodai kuwa alikuwa ameiba.