26th November, 2018
Mamlaka ya uchukuzi ikiongozwa na Francis Meja,imewataka wenye magari kuhakikisha kuwa wameweka vifaa vya kudhibiti mwendo vitakavyo sambaza takwimu za mwendo,wanaotumia madereva moja kwa moja mpaka makao makuu ya shirika hilo kabla ya tarehe mosi disemba mwaka huu ili kuviimarisha vifaa wanavyotumia sasa kabla ya machi mosi mwaka ujao. Wenye magari wanatakiwa kuhakikisha kuwa wamesanikisha vifaa hivi ili kuhakisha ubora wa viwango vya uchukuzi vinazingatiwa.wauzaji wa mitambo hii wametakiwa kufuata viwango vinavyohitajika na shirika la ukadiriaji ubora wa bidhaa kabla ya kupata leseni za kusambaza vifaa hivyo.meja alikuwa akiwahutubia wanahabari kwenye ofisi yake.