14th November, 2018
Mwanaharakati wa kisiasa na afisa mkuu wa maswala ya uchukuzi katika na ujenzi wa miradi ya umma katika Kaunti ya Nairobi Richard Mutinda Kavemba ameaga dunia baada ya kuugua kwa kipindi kifupi. Akitoa tangazo la kifo cha Kavemba, gavana wa Kaunti ya Nairobi Mike Sonko amesema kuwa Kavemba alikuwa amelazwa katika Hosipitali ya Nairobi siku chache zilizopita. Anakumbukwa kwa kushiriki kama mchambuzi katika kipindi cha maswala ya siasa cha Sunday Edition katika runinga ya KTN News kila siku ya jumapili.