8th October, 2018
Mwekezaji wa kibinafsi katika eneo la makongeni mjini thika amezua kizaazaa baada ya kutaka kituo cha polisi cha makongeni ambacho amedai kimejengwa katika ardhi yake kihamishwe mara moja. Taarifa zinasema kuwa mwekezaji huyo kupitia tume ya ardhi ?nlc amemwandikia barua ocs wa kituo hicho james mwita akitoa ilani ya kutaka polisi waondoke katika ardhi hiyo. Hata hivyo kamishna wa eneo la kati Wilson Njega pamoja na mbunge wa thika patrick wainaina wameapa kuwa kituo hicho hakitahamishwa na mwekezaji huyo.