×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mjane wa Aboud Rogo aachiliwa

5th October, 2018

Mjane wa aliyekuwa mhubiri wa Kiislamu Aboud Rogo, Haniya Sagar amewachiliwa huru baada ya kuhukimiwa kifungo cha miaka kumi gerezani kwa kuhusishwa na shambulio la kigaidi katika kituo kimoja cha polisi mjini Mombasa mwaka 2016. 

Mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu, hania alikata rufaa dhidi ya hukumu hiyo iliyotolewa hakimu wa mahakama ya Mombasa, Diana Mochache baada ya kupatikana na hatia ya kutotoa taarifa kuhusu magaidi waliokivamia kituo hicho cha polisi.

Katika uamuzi wake, hakimu Mochache alisema hania alikuwa akiwasiliana mara kawa mara na magaidi hao watatu; Tasnim Yakub, Ramla Abdirahman Hussein na Maimuna Abdirahman ambao waliuwawa na maafisa wa polisi dakika chache baada ya kuvamia kituo cha polisi cha Central. 

Mumewe Aboud Rogo aliuwawa na watu wasiojulikana Agosti mwaka 2012 na alidaiwa kuhusishwa na visa vya kigaidi nchini pamoja na mtandao wa Al Quaeda.

.
RELATED VIDEOS