5th October, 2018
Wanamuziki, jamaa na marafiki wa mwendazake malenga wa miziki ya lugha ya kikuyu joseph kamaru wanaendelea kuomboleza kifo cha mwanamuziki huyo aliyeaga dunia akiwa na umri wa miaka 79. kamaru alifariki mwendo wa saa tatu usiku hapo jana katika hospitali ya mp shah alikokuwa akipokea matibabu kutokana na ugonjwa wa maumivu ya mifupa almaarufu kama parkinson. cecilia wakesho na taarifa zaidi.