5th October, 2018
Polisi mjini eldoret wameanzisha uchunguzi kuhusu kifo cha mwanamke mmoja
ambaye anadaiwa kuuawa kwa kudungwa kisu na mwanamke mwenzake katika mtaa wa chebarus eneo la kesses. Haijafahamika ni kwa nini mwanamke huyo alifanya kitendo hicho. Edgar birgen ambaye ameishi kwenye ndoa na mwendazake monicah birgen kwa zaidi ya miaka 18, anasema sasa amesalia na mzigo wa kuwalea watoto bila mama yao. sasa ombi lake ni kwa vyombo vya usalama kutegua kitendawili cha mauaji ya mkewe na kumkabili mhusika kisheria.