24th September, 2018
Wakazi wa eneo la wangige huko kabete kaunti ya kiambu asubuhi ya leo waliupata mwili wa mwanamume mmoja ukiwa bila majeraha yoyote. Wapangaji waliukuta mwili huo na kuita polisi, kikiwa kisa cha pili ndani ya majuma mawili, ambapo msichana mwenye akili taahira alibakwa na kuuawa mita chache tu kutoka eneo hilo. Mwili wa mwanamume huyo ulipelekwa katika hifadhi ya maiti ya city, hapa nairobi.