24th September, 2018
Wanawake huko lodwar wakiongozwa na mwakilishi wa kike kaunti ya turkana Joyce Emanikor hapo jana walifanya maandamano wakitaka kukamatwa mara moja kwa jangili mmoja aliyem'baka na kumuua msichana wa umri wa miaka saba juma lililopita. polisi wamelaumiwa kwa kujikokota katika kuwakamata washukiwa wanaotenda maovu, huku wahudumu wa bodaboda wakiwa washukiwa wakuu wanaotumiwa kutenda uhalifu katika mji huo nyakati za usiku.