23rd September, 2018
Dismas Ewet na Peris Cherono waliibuka washindi wa makala ya mwaka huu ya mbio za Mombasa yaliyoandaliwa katika kaunti hiyo.
Ewek aliandikisha mda wa masaa mawili dakika 16 sekunde 52 na kushinda mbio za wanaume huku Arit Kigen akimaliza katika nafasi ya pili naye Abraham Too akachukua nafasi ya tatu.
Katika upande wa kina dada Peris Cherono aliandikia mda wa masaa mawili dakika 30 sekunde 44.
Alice Mogire alichukua nafasi ya pili huku Elizabeth Rumukol alichukua nafasi ya tatu.