23rd September, 2018
Timu ya Kariobangi Sharks ilifuzu fainali ya kombe la FKF Shield Cup baada ya kuilaza Ulinzi Stars mabao 4 1 katika mechi ya nusu fainali iliyochezewa ugani Kasarani.
Mabao ya Sharks yalifungwa na Abuya,Shaphan Oyugi naye Eric Kapaito akafunga mawili.
Cliff kasuti alifungia Ulinzi Stars bao la kufutia machozi kunako dakika ya 90.
Kwenye nusu fainali nyingine ambayo ilichezwa hii leo SOFAPAKA iliwalaza mabingwa AFC Leopards bao 1 0 na kufuzu kwenye fainali.
Bao la SOFAPAKA lilitiwa kimyani na Ellie Asieche.