22nd September, 2018
Mbunge wa Kandara Alice Wahome amewaomba viongozi kutoka Murang'a kuingilia kati mzozo unaoshuhudiwa katika kaunti hiyo.
Ni mzozo unaohusisha usimamizi wa kampuni za maji za Murang'a na Gavana wa kaunti hiyo Mwangi wa Iria.
Wahome alikuwa akizungumza katika hafla huko Laikipia.
Mzozo baina ya Gavana na wasimamizi wa kampuni za maji umechangia kukosekana kwa huduma za maji, jambo lililosababisha maandano mara kadhaa mjini Murang'a.