21st September, 2018
Jaji mkuu David Maraga amewaongoza majaji na mahakimu katika uzinduzi wa wa kitabu cha muongozo wa kushughulikia kesi za jinai nchini maarufu criminal procedure bench book.
Kitabu hiki kitatoa muongozo wa kusikilizwa na kuamuliwa kwa kesi za jinai katika muda mfupi zaidi iwezekanavyo.
Kitabu hiki kimezinduliwa baada ya jopo kuundwa mwaka jana ili kuangalia changamoto za kushughulikia kesi za aina hii.
Aidha kitabu hiki kitatumika kama muongozo wa mafunzo na utafiti katika maswala ya haki na sheria.