×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Gavana Obado ahojiwa na polisi kwa mara nyingine

21st September, 2018

Gavana wa kaunti ya Migori Okoth Obado amehojiwa katika makao makuu ya idara ya upelelezi hapa jijini Nairobi, kuhusiana na kifo cha Sharon Otieno. 

Obado alijiwasilisha katika afisi hizo mapema hii leo baada ya kupokea mwito. Haya yanajiri siku moja baada ya matokeo ya vinasaba yaani DNA kubainisha kuwa ujauzito wa Sharon ulikuwa wa Obado. 

Sharon alikuwa na uja uzito wa miezi saba alipokumbana na mauti yake. Hii ni mara ya pili kuhojiwa kwa gavana huyo.  

Ikumbukwe msaidizi wa Gavana Obado Michael Oyamo na aliyekuwa mwakilishi wa wadi wa Kanyadoto Lawrence Mula ni miongoni mwa washukiwa wakuu wa mauaji hayo, wanaendelea kuzuiliwa. 

Mwili wa Sharon ulipatikana tarehe tano mwezi huu. 

.
RELATED VIDEOS