21st September, 2018
Seneta wa baringo Gideon Moi hii leo amezindua rasmi mradi wa mashine ya kuchuja na kusafisha maji kwa mimea inaogarimu shilingi milioni kumi na nane katika county ndogo ya nakuru eneo la rongai. Mashine hiyo iliyozinduliwa inauwezo wa kuzilisha maji kwa kiwango kikubwa ambapo maji yatakayozalishwa kwa siku moja yatatosheleza matumizi ya wiki moja. Hata hivyo seneta amesema kuwa mradi hua utasaidia ukuzaji na ustawishaji wa mimea kwa haraka. Aidha amewataka viongozi kutoka sehemu kame kuanzisha mradi huo ili kuepukana na tatizo la maji. Hafla hiyo ya uzinduzi ilihudhuriwa na rais mstaafu Daniel Arap Moi pamoja na balozi wa Israel Noah Gal Gendler.