.
19th September, 2018
Ziara ya ghafla ya gavana wa Nairobi Mike Sonko katika hospitali ya Pumwani sasa inaendelea kufichua mapungufu katika kituo hicho kilicho na uwezo wa kulaza wagonjwa 415 kwa wakati mmoja. Haya yanajiri huku baadhi ya maseneta waliozuru kituo hicho wakidokeza haja ya kugeuza usimamizi wa hospitali hiyo kutoka kaunti hadi ule wa kitaifa. Kisa hiki kinajiri huku wakosoaji wa gavana wa Nairobi wakilaumu Utawala wake kwa kutozingatia utendakazi wa vituo muhimu vya afya Nairobi ikiwemo hiyo hospitali ya Pumwani.