.
18th September, 2018
Hatimae Spika wa Bunge la Kitaifa Justin Muturi amewasilisha ujumbe wa Rais Bungeni kuhusu pendekezo lake ya mswada wa fedha wa mwaka wa 2018 ufanyiwe marekebisho tena ili kupunguza kiwango cha kodi itakayotozwa bidhaa za mafuta kutoka asilimia 16 hadi asilimia nane. Hata hivyo wabunge ambao isemekana wanajiandaa kutupilia mbali pendekezo la rais licha ya vinara wa mirengo ya jubilee na nasa kuwataka waunge mkono. Mwanahabari wetu mwandamizi na mjuzi katika maswala haya ya siasa duncan khaemba anashuka na taarifa hiyo.