18th September, 2018
Kwa wakazi wa taita taveta, ipo afueni katika sekta ya afya baada ya serikali ya kaunti kuleta mashine ya kupima viungo vya ndani ya mwili, maarufu kama ct scan. Mashine hiyo mpya ina uwezo wa kuwahudumia wagonjwa ishirini kila siku, ikiwa na teknolojia ya kunakili na kurekodi picha kwa wiki moja. Wenyeji wamekuwa wakisafiri hadi mombasa au nairobi kutafuta huduma za mashine hiyo. Waziri wa afya kaunti ya Taita taveta daktari frank mwangemi alizungumza kuhusu hatua zilizopigwa.