17th September, 2018
Familia moja inayoishi maisha ya uchochole huko ukunda kaunti ya kwale inataka haki kutokana na bwanyenye mmoja anayedai umiliki wa ekari tano za shamba lao. Mesali yussuf anasema mfanyabiashara huyo anawataka kuhama kutoka shamba hilo ambalo ni la baba marehemu baba yao, ambapo hawajawa na amani tangu kifo cha mzee wao mwaka wa 2010. mkurugenzi wa shirika la genesis for human rights commission Caleb Ngwena, anataka serikali kuingilia kati, ili familia hiyo ipate haki.