.
17th September, 2018
Wakazi wa mtaa wa maili tatu katika mpaka wa Isiolo na Meru wanalilia haki baada ya Uvamizi wa alfajiri ambapo nyumba tisa ziliteketezwa. walioshuhudia kisa hicho wanasema wenyeji walikimbia kwa kuogopa mlio wa risasi kutoka kwa wavamizi hao wanaokisiwa walikuwa arobaini kwa idadi. Wanaamini sababu ya shambulizi hilo ni tamaa ya ardhi kwani hawakuiba chochote. sasa wanaitaka tume ya ardhi nchini nlc na kiongozi wa mashtaka ya umma kuchukua hatua mwafaka ili wapate haki.