16th September, 2018
Viongozi katika kaunti ya Mombasa wamelalamikia ongezeko la magenge ya uhalifu mjini Mombasa na kutoa wito wa kufufuliwa kwa mpango wa nyumba kumi.
Viongozi hao kutoka kwa kamati ya amani Mombasa wakiongozwa na mbunge wa Mvita Abdulswamad Shariff Nassir wamelaani mauaji ya kiholela katika mji wa Mombasa na kuitaka serikali kutofanya mageuzi katika idara ya polisi kwa pupa.