10th September, 2018
Wafanyabiashara na watumizi wa barabara ya nairobi ? nakuru haswa eneo la kiambu sasa wanakumbwa na tatizo la ukosefu wa maji safi, ukosefu wa vyoo na pia ukosefu wa mitaro ya maji taka ni hali ambayo inawalazimisha watumizi wa barabar hiyo wakati mwingi kujisaidia ndani ya misitu iliyoko kando ya barabara. matatizo zaidi yanaibuka wakati wa mvua ambapo uchafu wote unaelekezwa mitoni na kuwa chanzo cha magonjwa. wafanyibiashara wanalalamika kuwa licha ya kuwa waaminifu katika kutoa ushuru, serikali ya kaunti haijazingatia mahitaji hayo muhimu.