9th September, 2018
Gavana wa kaunti ya nairobi ameendelea kutetea uamuzi wake wa kufanyia kazi nyumbani kwake katika kaunti ya machakos licha ya lalama za waakilishi wa wadi ambao baadhi wametishia kuwasilisha hoja ya kutimua katika bunge la kaunti hiyo. akizungumza katika sherehe ya kumbukumbu miaka mitatu tangu kifo cha babake, sonko anasema kuwa tofauti zilizopo katika bunge la kaunti zinashughulikiwa na viongozi wa kaunti ya nairobi .