6th September, 2018
Timu ya Gofu ya wanawake wa Tanzania imepokelewa jijini Dar es Salaam baada ya kuibuka washindi wa pili katika mashindano ya kombe la chalenji ya Afrika kwa mchezo wa gofu wanawake uliohusisha nchi kumi na nane (18) yaliyofanyika kati ya Agosti 29 na Septemba 4 mwaka huu mjini accra ghana ambapo nafasi ya kwanza ilichukuliwa na afrika kusini.
Timu hiyo ya tanzanja yenye wachezaji wanne pia imetoa mchezaji bora Afrika wa mashindano hayo anayeitwa Madina Iddy na Tanzania itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo mwaka 2022.