6th September, 2018
Muungano wa wanawake katika bunge la kaunti ya Migori umelaani vikali mauaji ya mwanafunzi wa chuo kikuu cha Rongo Sharon Otieno.
Mwenyekiti wa muungano huo Florence Oile amewaongoza wenzake kutoa wito kwa polisi kuharakisha uchunguzi na kuwakamata wahusika. wamezungumza mapema leo mjini Migori.