2nd September, 2018
Seneta wa kaunti ya baringo gideon moi anaitaka serikali kuahirisha utekelezaji wa 16% ya ushuru wa ziada unaotozwa bidhaa za petroli ambao umesababisha ongezeko kubwa la bei ya mafuta nchini. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, seneta moi ametaka serikali kutafuta mbinu mbadala za kukusanya kodi baada ya kuwawekea kenya mzigo. Amesema ongezeko la bei ya mafuta litaongeza gharama ya maisha kwa wakenya wengi. Baada ya utekelezaji wa sheria hiyo sasa bei ya mafuta ya petroli mjini mombasa ni shilingi 124 na senti 49 huku mjini Nairobi mafuta hayo yakiuzwa kwa shilingi 127 na senti 80.Mjini mandera mafuta ya petroli yanauzwa kwa shilingi 141 na senti 6 kwa lita.